×

Nawapewe mafakiri walio zuilika katika njia za Mwenyezi Mungu, wasio weza kusafiri 2:273 Swahili translation

Quran infoSwahiliSurah Al-Baqarah ⮕ (2:273) ayat 273 in Swahili

2:273 Surah Al-Baqarah ayat 273 in Swahili (السواحيلية)

Quran with Swahili translation - Surah Al-Baqarah ayat 273 - البَقَرَة - Page - Juz 3

﴿لِلۡفُقَرَآءِ ٱلَّذِينَ أُحۡصِرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا يَسۡتَطِيعُونَ ضَرۡبٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ يَحۡسَبُهُمُ ٱلۡجَاهِلُ أَغۡنِيَآءَ مِنَ ٱلتَّعَفُّفِ تَعۡرِفُهُم بِسِيمَٰهُمۡ لَا يَسۡـَٔلُونَ ٱلنَّاسَ إِلۡحَافٗاۗ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٌ ﴾
[البَقَرَة: 273]

Nawapewe mafakiri walio zuilika katika njia za Mwenyezi Mungu, wasio weza kusafiri katika nchi kutafuta riziki. Asiye wajua hali zao huwadhania kuwa ni matajiri kwa sababu ya kujizuia kwao. Utawatambua kwa alama zao; hawang'ang'analii watu kwa kuwaomba. Na kheri yoyote mnayo toa, basi kwa yakini Mwenyezi Mungu anaijua

❮ Previous Next ❯

ترجمة: للفقراء الذين أحصروا في سبيل الله لا يستطيعون ضربا في الأرض يحسبهم, باللغة السواحيلية

﴿للفقراء الذين أحصروا في سبيل الله لا يستطيعون ضربا في الأرض يحسبهم﴾ [البَقَرَة: 273]

Abdullah Muhammad Abu Bakr
Wapeni sadaka zenu mafukara Waislamu ambao hawawezi kusafiri kutafuta riziki, kwa kuwa wameshughulika na jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, ambao huwadhania wao wasiowajua kuwa hawahitaji sadaka kwa kuwa wamejizuia na kuomba.Utawajua kwa alama zao na athari ya uhitaji walionao. Hawaombi kabisa. Na wakiomba, kwa kukosa budi, hawaombi kwa utiriri. Na mali yoyote mnayoyatoa katika njia ya Mwenyezi Mungu, hakuna chochote, katika hayo, chenye kufichika kwa Mwenyezi Mungu.Na Mwenyezi Mungu Atalipa kwayo malipo mengi zaidi na makamilifu zaidi Siku ya Kiyama
❮ Previous Next ❯

Verse in more languages

Transliteration Bangla Bosnian German English Persian French Hindi Indonesian Kazakh Dutch Russian Spanish Turkish Urdu Uzbek