×

Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenyezi Mungu, ambaye ameziumba mbingu na ardhi 10:3 Swahili translation

Quran infoSwahiliSurah Yunus ⮕ (10:3) ayat 3 in Swahili

10:3 Surah Yunus ayat 3 in Swahili (السواحيلية)

Quran with Swahili translation - Surah Yunus ayat 3 - يُونس - Page - Juz 11

﴿إِنَّ رَبَّكُمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ يُدَبِّرُ ٱلۡأَمۡرَۖ مَا مِن شَفِيعٍ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ إِذۡنِهِۦۚ ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُ رَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُوهُۚ أَفَلَا تَذَكَّرُونَ ﴾
[يُونس: 3]

Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenyezi Mungu, ambaye ameziumba mbingu na ardhi kwa siku sita, na ametawala kwenye ufalme wake, anaendesha mambo yote. Hapana mwombezi ila baada ya idhini yake. Huyo ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Je! Hamkumbuki

❮ Previous Next ❯

ترجمة: إن ربكم الله الذي خلق السموات والأرض في ستة أيام ثم استوى, باللغة السواحيلية

﴿إن ربكم الله الذي خلق السموات والأرض في ستة أيام ثم استوى﴾ [يُونس: 3]

Abdullah Muhammad Abu Bakr
Hakika Mola wenu ni Mwenyezi Mungu Ambaye Alizipatisha mbingu na ardhi katika kipindi cha Siku Sita, kisha Akalingana, yaani Akawa juu ya 'Arsh, mlingano unaonasibiana na utisho Wake na utukufu Wake. Anaendesha mambo ya viumbe Vyake. Hakuna yoyote Anayempinga katika uamuzi Wake na hakuna muombezi yoyote anayeombea mbele Yake Siku ya Kiyama isipokuwa baada ya Yeye kumpa idhini kuombea. Basi muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wenu, Anayesifika kwa sifa hizi na mtakasiyeni ibada. Je, hamwaidhiki na mkazizingatia aya hizi na hoja
❮ Previous Next ❯

Verse in more languages

Transliteration Bangla Bosnian German English Persian French Hindi Indonesian Kazakh Dutch Russian Spanish Turkish Urdu Uzbek