×

Na Dhun-Nun alipoondoka hali ameghadhibika, na akadhani ya kwamba hatutakuwa na uwezo 21:87 Swahili translation

Quran infoSwahiliSurah Al-Anbiya’ ⮕ (21:87) ayat 87 in Swahili

21:87 Surah Al-Anbiya’ ayat 87 in Swahili (السواحيلية)

Quran with Swahili translation - Surah Al-Anbiya’ ayat 87 - الأنبيَاء - Page - Juz 17

﴿وَذَا ٱلنُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَٰضِبٗا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقۡدِرَ عَلَيۡهِ فَنَادَىٰ فِي ٱلظُّلُمَٰتِ أَن لَّآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنتَ سُبۡحَٰنَكَ إِنِّي كُنتُ مِنَ ٱلظَّٰلِمِينَ ﴾
[الأنبيَاء: 87]

Na Dhun-Nun alipoondoka hali ameghadhibika, na akadhani ya kwamba hatutakuwa na uwezo juu yake. Basi aliita katika giza: Hapana mungu isipo kuwa Wewe Subhanaka Uliye takasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa wenye kudhulumu

❮ Previous Next ❯

ترجمة: وذا النون إذ ذهب مغاضبا فظن أن لن نقدر عليه فنادى في, باللغة السواحيلية

﴿وذا النون إذ ذهب مغاضبا فظن أن لن نقدر عليه فنادى في﴾ [الأنبيَاء: 87]

Abdullah Muhammad Abu Bakr
Na kumbuka kisa cha mtu wa chewa, naye ni Yūnus mwana wa Mattā, amani imshukie, Mwenyezi Mungu Alimtumiliza kwa watu wake, akawalingania wasimuamini, akawaonya kuwa wataadhibiwa, lakikni hawakurudi nyuma. Na asiwavumilie kama vile Mwenyezi Mungu Alivyomuamrisha na akaondoka kutoka kwao akiwa na hasira juu yao, akiwa amebanwa na kifua kwa kuasi kwao. Na akadhani kwamba Mwenyezi Mungu Hatampa dhiki na kumuadhibu kwa ukiukaji huu. Mwenyezi Mungu Akamtahini kwa dhiki nyingi na kifungo na akamezwa na tewa baharini, na akamlingania Mola wake kwa kumuomba katika magiza ya usiku, bahari na tumbo la tewa hali ya kutubia na kukubali ukiukaji wake kwa kuacha kuwavumilia watu wake, huku akisema, «Hapana muabudiwa kwa haki isipokuwa wewe! Kutakasika na sifa za upungufu ni kwako! kwa hakika mimi nimekuwa miongoni mwa wenye kudhulumu!»
❮ Previous Next ❯

Verse in more languages

Transliteration Bangla Bosnian German English Persian French Hindi Indonesian Kazakh Dutch Russian Spanish Turkish Urdu Uzbek