The Quran in Swahili - Surah Inshiqaq translated into Swahili, Surah Al-Inshiqaq in Swahili. We provide accurate translation of Surah Inshiqaq in Swahili - السواحيلية, Verses 25 - Surah Number 84 - Page 589.

| إِذَا السَّمَاءُ انشَقَّتْ (1) Itapo chanika mbingu | 
| وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ (2) Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza | 
| وَإِذَا الْأَرْضُ مُدَّتْ (3) Na ardhi itakapo tanuliwa | 
| وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ (4) Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu | 
| وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ (5) Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza | 
| يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًا فَمُلَاقِيهِ (6) Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta | 
| فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ (7) Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia | 
| فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا (8) Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi | 
| وَيَنقَلِبُ إِلَىٰ أَهْلِهِ مَسْرُورًا (9) Na arudi kwa ahali zake na furaha | 
| وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ وَرَاءَ ظَهْرِهِ (10) Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake | 
| فَسَوْفَ يَدْعُو ثُبُورًا (11) Basi huyo ataomba kuteketea | 
| وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا (12) Na ataingia Motoni | 
| إِنَّهُ كَانَ فِي أَهْلِهِ مَسْرُورًا (13) Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake | 
| إِنَّهُ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ (14) Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena | 
| بَلَىٰ إِنَّ رَبَّهُ كَانَ بِهِ بَصِيرًا (15) Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona | 
| فَلَا أُقْسِمُ بِالشَّفَقِ (16) Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa | 
| وَاللَّيْلِ وَمَا وَسَقَ (17) Na kwa usiku na unavyo vikusanya | 
| وَالْقَمَرِ إِذَا اتَّسَقَ (18) Na kwa mwezi unapo pevuka | 
| لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٍ (19) Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka | 
| فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ (20) Basi wana nini hawaamini | 
| وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ الْقُرْآنُ لَا يَسْجُدُونَ ۩ (21) Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu | 
| بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا يُكَذِّبُونَ (22) Bali walio kufuru wanakanusha tu | 
| وَاللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ (23) Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria | 
| فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ (24) Basi wabashirie adhabu chungu | 
| إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ (25) Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika |