Quran with Swahili translation - Surah At-Tahrim ayat 12 - التَّحرِيم - Page - Juz 28
﴿وَمَرۡيَمَ ٱبۡنَتَ عِمۡرَٰنَ ٱلَّتِيٓ أَحۡصَنَتۡ فَرۡجَهَا فَنَفَخۡنَا فِيهِ مِن رُّوحِنَا وَصَدَّقَتۡ بِكَلِمَٰتِ رَبِّهَا وَكُتُبِهِۦ وَكَانَتۡ مِنَ ٱلۡقَٰنِتِينَ ﴾
[التَّحرِيم: 12]
﴿ومريم ابنة عمران التي أحصنت فرجها فنفخنا فيه من روحنا وصدقت بكلمات﴾ [التَّحرِيم: 12]
Abdullah Muhammad Abu Bakr Na Mwenyezi Mungu Anapiga mfano kwa walioamini. Mfano wenyewe ni Maryam binti 'Imran aliyeihifadhi tupu yake na akailinda na uzinifu, basi mwenyezi Mungu Akamuamrisha Jibrili, amani imshukie, apulize kwenye mfuko wa nguo yake. Na ule mpulizo ukafika kwenye uzao wake. Hapo akabeba mimba ya ‘Īsā, amani imshukie, akayaamini maneno ya Mola wake, akafuata kivitendo Sheria Zake Alizozipasisha kwa waja Wake na vitabu Vyake Alivyoviteremsha kwa Mitume Wake, na akawa ni miongoni mwa wale wenye kumtii Yeye |