Quran with Swahili translation - Surah Al-A‘raf ayat 126 - الأعرَاف - Page - Juz 9
﴿وَمَا تَنقِمُ مِنَّآ إِلَّآ أَنۡ ءَامَنَّا بِـَٔايَٰتِ رَبِّنَا لَمَّا جَآءَتۡنَاۚ رَبَّنَآ أَفۡرِغۡ عَلَيۡنَا صَبۡرٗا وَتَوَفَّنَا مُسۡلِمِينَ ﴾
[الأعرَاف: 126]
﴿وما تنقم منا إلا أن آمنا بآيات ربنا لما جاءتنا ربنا أفرغ﴾ [الأعرَاف: 126]
Abdullah Muhammad Abu Bakr «Na wewe hukutupata na jambo lolote la kutuaibisha na kutupinga kwalo, ewe Fir'awn, isipokuwa ni kule kuamini kwetu na kukubali kwetu hoja za Mola wetu na dalili Zake alizokuja nazo Mūsā ambazo wewe huwezi kuleta mfano wake wala yoyote mwingine asiyekuwa Mwenyezi Mungu Ambaye ni Yake mamlaka ya mbingu na ardhi. Mola wetu! Tumiminie subira kubwa na uthabiti juu yake, na utufishe tukiwa ni wenye kwndama amri yako, wenye kumfuata Mtume wako.» |