×

Yeye ndiye aliye lijaalia jua kuwa na mwangaza, na mwezi ukawa na 10:5 Swahili translation

Quran infoSwahiliSurah Yunus ⮕ (10:5) ayat 5 in Swahili

10:5 Surah Yunus ayat 5 in Swahili (السواحيلية)

Quran with Swahili translation - Surah Yunus ayat 5 - يُونس - Page - Juz 11

﴿هُوَ ٱلَّذِي جَعَلَ ٱلشَّمۡسَ ضِيَآءٗ وَٱلۡقَمَرَ نُورٗا وَقَدَّرَهُۥ مَنَازِلَ لِتَعۡلَمُواْ عَدَدَ ٱلسِّنِينَ وَٱلۡحِسَابَۚ مَا خَلَقَ ٱللَّهُ ذَٰلِكَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۚ يُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ ﴾
[يُونس: 5]

Yeye ndiye aliye lijaalia jua kuwa na mwangaza, na mwezi ukawa na nuru, na akaupimia vituo ili mjue idadi ya miaka na hisabu. Mwenyezi Mungu hakuviumba hivyo ila kwa Haki. Anazipambanua Ishara kwa watu wanao jua

❮ Previous Next ❯

ترجمة: هو الذي جعل الشمس ضياء والقمر نورا وقدره منازل لتعلموا عدد السنين, باللغة السواحيلية

﴿هو الذي جعل الشمس ضياء والقمر نورا وقدره منازل لتعلموا عدد السنين﴾ [يُونس: 5]

Abdullah Muhammad Abu Bakr
Mwenyezi Mungu Ndiye ambaye Alilifanya jua kuwa d,iyā’ (mwangaza), Akaufanya mwezi kuwa ni nūr (mng’aro) na Akaupangia mwezi njia zake za kupita. Ikawa kwa jua zinajulikana siku, na kwa mwezi inajulikana miezi na miaka. Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Hakuumba jua na mwezi isipokuwa ni hekima kubwa, na kuonesha ukamilifu wa uwezo wa Mwenyezi Mungu na ujuzi Wake; Anafafanua hoja na dalili kwa watu wanaojua hekima ya utengenezaji wa uumbaji
❮ Previous Next ❯

Verse in more languages

Transliteration Bangla Bosnian German English Persian French Hindi Indonesian Kazakh Dutch Russian Spanish Turkish Urdu Uzbek