Quran with Swahili translation - Surah Yunus ayat 89 - يُونس - Page - Juz 11
﴿قَالَ قَدۡ أُجِيبَت دَّعۡوَتُكُمَا فَٱسۡتَقِيمَا وَلَا تَتَّبِعَآنِّ سَبِيلَ ٱلَّذِينَ لَا يَعۡلَمُونَ ﴾
[يُونس: 89]
﴿قال قد أجيبت دعوتكما فاستقيما ولا تتبعان سبيل الذين لا يعلمون﴾ [يُونس: 89]
Abdullah Muhammad Abu Bakr Akasema Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kuwambia wao wawili, «Yameshakubaliwa maombi yenu juu ya Fir'awn na kundi lake na mali zao,- Mūsā alikuwa akiomba, na Hārūn akiitika maombi yake, ndipo ikafaa kuyanasibisha maombi kwa wao wawili,- basi jikiteni kwenye Dini yenu na muendelee kumlingania Fir'awn na watu wake kwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kumtii, na msifuate njia ya asiyejua ahadi yangu njema na onyo langu.» |