×

Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita; kisha akakaa 57:4 Swahili translation

Quran infoSwahiliSurah Al-hadid ⮕ (57:4) ayat 4 in Swahili

57:4 Surah Al-hadid ayat 4 in Swahili (السواحيلية)

Quran with Swahili translation - Surah Al-hadid ayat 4 - الحدِيد - Page - Juz 27

﴿هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ يَعۡلَمُ مَا يَلِجُ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا يَخۡرُجُ مِنۡهَا وَمَا يَنزِلُ مِنَ ٱلسَّمَآءِ وَمَا يَعۡرُجُ فِيهَاۖ وَهُوَ مَعَكُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ ﴾
[الحدِيد: 4]

Yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita; kisha akakaa vyema juu ya enzi. Anayajua yanayo ingia katika ardhi na yanayo toka humo, na yanayo teremka kutoka mbinguni, na yanayo panda humo. Naye yu pamoja nanyi popote mlipo. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona mnayo yatenda

❮ Previous Next ❯

ترجمة: هو الذي خلق السموات والأرض في ستة أيام ثم استوى على العرش, باللغة السواحيلية

﴿هو الذي خلق السموات والأرض في ستة أيام ثم استوى على العرش﴾ [الحدِيد: 4]

Abdullah Muhammad Abu Bakr
Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi kisha Akawa juu ya 'Arsh Yake iliyo juu ya viumbe Vyake vyote kuwa Juu kunakonasibiana na utukufu Wake. Anavijua vinavyoingia ardhini, miongoni mwa mbegu, mvua na visivyokuwa hivyo, na vinavyotoka humo miongoni mwa mimea, nafaka na matunda, na vinavyoshuka kutoka mbinguni, miongoni mwa mvua na vinginevyo, na vinvyopanda huko, miongoni mwa Malaika na matendo ( ya awaja), na Yeye , kutakasika ni Kwake, Yuko pamoja na nyinyi kwa ujuzi Wake popote mnapokuwa. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyaona matendo yenu mnayoyafanya na Atawalipa kwayo
❮ Previous Next ❯

Verse in more languages

Transliteration Bangla Bosnian German English Persian French Hindi Indonesian Kazakh Dutch Russian Spanish Turkish Urdu Uzbek