×

Mwenyezi Mungu atasema: Ingieni Motoni pamoja na umma zilizo pita kabla yenu 7:38 Swahili translation

Quran infoSwahiliSurah Al-A‘raf ⮕ (7:38) ayat 38 in Swahili

7:38 Surah Al-A‘raf ayat 38 in Swahili (السواحيلية)

Quran with Swahili translation - Surah Al-A‘raf ayat 38 - الأعرَاف - Page - Juz 8

﴿قَالَ ٱدۡخُلُواْ فِيٓ أُمَمٖ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِكُم مِّنَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِ فِي ٱلنَّارِۖ كُلَّمَا دَخَلَتۡ أُمَّةٞ لَّعَنَتۡ أُخۡتَهَاۖ حَتَّىٰٓ إِذَا ٱدَّارَكُواْ فِيهَا جَمِيعٗا قَالَتۡ أُخۡرَىٰهُمۡ لِأُولَىٰهُمۡ رَبَّنَا هَٰٓؤُلَآءِ أَضَلُّونَا فَـَٔاتِهِمۡ عَذَابٗا ضِعۡفٗا مِّنَ ٱلنَّارِۖ قَالَ لِكُلّٖ ضِعۡفٞ وَلَٰكِن لَّا تَعۡلَمُونَ ﴾
[الأعرَاف: 38]

Mwenyezi Mungu atasema: Ingieni Motoni pamoja na umma zilizo pita kabla yenu za majini na watu. Kila utakapo ingia umma utawalaani wenzake. Mpaka watakapo kusanyika wote humo, wa mwisho wao watawasema wa mwanzo wao: Mola wetu Mlezi! Hawa ndio walio tupoteza; basi wape adhabu ya Motoni marudufu. Atasema: Itakuwa kwenu nyote marudufu, lakini nyinyi hamjui tu

❮ Previous Next ❯

ترجمة: قال ادخلوا في أمم قد خلت من قبلكم من الجن والإنس في, باللغة السواحيلية

﴿قال ادخلوا في أمم قد خلت من قبلكم من الجن والإنس في﴾ [الأعرَاف: 38]

Abdullah Muhammad Abu Bakr
Hapo Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Atasema kuwaambia washirikina hawa wazushi, «Ingieni Motoni mkiwa pamoja na makundi ya walio mfano wenu katika ukafiri, waliotangulia kabla yenu, kati ya majini na wanadamu. Kila kundi la mila mimoja likiingia Motoni litalaani watu wa kundi lingine linalofanana nalo, waliokuwa ni sababu ya kupotea kwake kwa kuwafuata. Mpaka watakapokutana ndani ya Moto wote pamoja: wa mwanzo, miongoni mwa wafuasi wa mila za kikafiri, na wa mwisho miongoni mwao; hapo watasema wa mwisho, waliokuwa ni watu wa kuandama ulimwenguni, kuwaambia viongozi wao, «Mola wetu, hawa ndio waliotupoteza wakatupotosha na haki, basi wape adhabu nyongeza ya Moto.» Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Atasema, «Kila mmoja atapata nyongeza.» Yaani, kila mmoja kati yenu na wao atapata adhabu nyongeza ya Moto, «lakini nyinyi wafuasi hamuijui ile sehemu ya adhabu na machungu ambayo kila kundi miongoni mwenu ataipata.»
❮ Previous Next ❯

Verse in more languages

Transliteration Bangla Bosnian German English Persian French Hindi Indonesian Kazakh Dutch Russian Spanish Turkish Urdu Uzbek