×

Surah Al-Waqiah in Swahili

Quran Swahili ⮕ Surah Waqiah

Translation of the Meanings of Surah Waqiah in Swahili - السواحيلية

The Quran in Swahili - Surah Waqiah translated into Swahili, Surah Al-Waqiah in Swahili. We provide accurate translation of Surah Waqiah in Swahili - السواحيلية, Verses 96 - Surah Number 56 - Page 534.

بسم الله الرحمن الرحيم

إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ (1)
Litakapo tukia hilo Tukio
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ (2)
Hapana cha kukanusha kutukia kwake
خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ (3)
Literemshalo linyanyualo
إِذَا رُجَّتِ الْأَرْضُ رَجًّا (4)
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso
وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسًّا (5)
Na milima itapo sagwasagwa
فَكَانَتْ هَبَاءً مُّنبَثًّا (6)
Iwe mavumbi yanayo peperushwa
وَكُنتُمْ أَزْوَاجًا ثَلَاثَةً (7)
Na nyinyi mtakuwa namna tatu
فَأَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ (8)
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani
وَأَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ (9)
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni
وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ (10)
Na wa mbele watakuwa mbele
أُولَٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ (11)
Hao ndio watakao karibishwa
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ (12)
Katika Bustani zenye neema
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ (13)
Fungu kubwa katika wa mwanzo
وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ (14)
Na wachache katika wa mwisho
عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ (15)
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa
مُّتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ (16)
Wakiviegemea wakielekeana
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ (17)
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele
بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ (18)
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ (19)
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa
وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ (20)
Na matunda wayapendayo
وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ (21)
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani
وَحُورٌ عِينٌ (22)
Na Mahurulaini
كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ (23)
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa
جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ (24)
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda
لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا (25)
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi
إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا (26)
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama
وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ (27)
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani
فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ (28)
Katika mikunazi isiyo na miba
وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ (29)
Na migomba iliyo pangiliwa
وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ (30)
Na kivuli kilicho tanda
وَمَاءٍ مَّسْكُوبٍ (31)
Na maji yanayo miminika
وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ (32)
Na matunda mengi
لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ (33)
Hayatindikii wala hayakatazwi
وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ (34)
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa
إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاءً (35)
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya
فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًا (36)
Na tutawafanya vijana
عُرُبًا أَتْرَابًا (37)
Wanapendana na waume zao, hirimu moja
لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ (38)
Kwa ajili ya watu wa kuliani
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ (39)
Fungu kubwa katika wa mwanzo
وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ (40)
Na fungu kubwa katika wa mwisho
وَأَصْحَابُ الشِّمَالِ مَا أَصْحَابُ الشِّمَالِ (41)
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni
فِي سَمُومٍ وَحَمِيمٍ (42)
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka
وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ (43)
Na kivuli cha moshi mweusi
لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ (44)
Si cha kuburudisha wala kustarehesha
إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ (45)
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa
وَكَانُوا يُصِرُّونَ عَلَى الْحِنثِ الْعَظِيمِ (46)
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa
وَكَانُوا يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ (47)
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ (48)
Au baba zetu wa zamani
قُلْ إِنَّ الْأَوَّلِينَ وَالْآخِرِينَ (49)
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ (50)
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu
ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ (51)
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha
لَآكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ (52)
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu
فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ (53)
Na kwa mti huo mtajaza matumbo
فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ (54)
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka
فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ (55)
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu
هَٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ (56)
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo
نَحْنُ خَلَقْنَاكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ (57)
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki
أَفَرَأَيْتُم مَّا تُمْنُونَ (58)
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza
أَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُ أَمْ نَحْنُ الْخَالِقُونَ (59)
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji
نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ (60)
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِي مَا لَا تَعْلَمُونَ (61)
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ (62)
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki
أَفَرَأَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ (63)
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda
أَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ (64)
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha
لَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَاهُ حُطَامًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ (65)
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu
إِنَّا لَمُغْرَمُونَ (66)
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ (67)
Bali sisi tumenyimwa
أَفَرَأَيْتُمُ الْمَاءَ الَّذِي تَشْرَبُونَ (68)
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa
أَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ الْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ الْمُنزِلُونَ (69)
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha
لَوْ نَشَاءُ جَعَلْنَاهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ (70)
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru
أَفَرَأَيْتُمُ النَّارَ الَّتِي تُورُونَ (71)
Je! Mnauona moto mnao uwasha
أَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَا أَمْ نَحْنُ الْمُنشِئُونَ (72)
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji
نَحْنُ جَعَلْنَاهَا تَذْكِرَةً وَمَتَاعًا لِّلْمُقْوِينَ (73)
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ (74)
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu
۞ فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ (75)
Basi naapa kwa maanguko ya nyota
وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ (76)
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua
إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ (77)
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu
فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ (78)
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ (79)
Hapana akigusaye ila walio takaswa
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ (80)
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote
أَفَبِهَٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ (81)
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza
وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ (82)
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha
فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ (83)
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo
وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ (84)
Na nyinyi wakati huo mnatazama
وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ (85)
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi
فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ (86)
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu
تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ (87)
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli
فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ (88)
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa
فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ (89)
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ (90)
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia
فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ (91)
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ (92)
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu
فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ (93)
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka
وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ (94)
Na kutiwa Motoni
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ (95)
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ (96)
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa
❮ Previous Next ❯

Surahs from Quran :

1- Fatiha2- Baqarah
3- Al Imran4- Nisa
5- Maidah6- Anam
7- Araf8- Anfal
9- Tawbah10- Yunus
11- Hud12- Yusuf
13- Raad14- Ibrahim
15- Hijr16- Nahl
17- Al Isra18- Kahf
19- Maryam20- TaHa
21- Anbiya22- Hajj
23- Muminun24- An Nur
25- Furqan26- Shuara
27- Naml28- Qasas
29- Ankabut30- Rum
31- Luqman32- Sajdah
33- Ahzab34- Saba
35- Fatir36- Yasin
37- Assaaffat38- Sad
39- Zumar40- Ghafir
41- Fussilat42- shura
43- Zukhruf44- Ad Dukhaan
45- Jathiyah46- Ahqaf
47- Muhammad48- Al Fath
49- Hujurat50- Qaf
51- zariyat52- Tur
53- Najm54- Al Qamar
55- Rahman56- Waqiah
57- Hadid58- Mujadilah
59- Al Hashr60- Mumtahina
61- Saff62- Jumuah
63- Munafiqun64- Taghabun
65- Talaq66- Tahrim
67- Mulk68- Qalam
69- Al-Haqqah70- Maarij
71- Nuh72- Jinn
73- Muzammil74- Muddathir
75- Qiyamah76- Insan
77- Mursalat78- An Naba
79- Naziat80- Abasa
81- Takwir82- Infitar
83- Mutaffifin84- Inshiqaq
85- Buruj86- Tariq
87- Al Ala88- Ghashiya
89- Fajr90- Al Balad
91- Shams92- Lail
93- Duha94- Sharh
95- Tin96- Al Alaq
97- Qadr98- Bayyinah
99- Zalzalah100- Adiyat
101- Qariah102- Takathur
103- Al Asr104- Humazah
105- Al Fil106- Quraysh
107- Maun108- Kawthar
109- Kafirun110- Nasr
111- Masad112- Ikhlas
113- Falaq114- An Nas