×

Surah Ar-Rahman in Swahili

Quran Swahili ⮕ Surah Rahman

Translation of the Meanings of Surah Rahman in Swahili - السواحيلية

The Quran in Swahili - Surah Rahman translated into Swahili, Surah Ar-Rahman in Swahili. We provide accurate translation of Surah Rahman in Swahili - السواحيلية, Verses 78 - Surah Number 55 - Page 531.

بسم الله الرحمن الرحيم

الرَّحْمَٰنُ (1)
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
عَلَّمَ الْقُرْآنَ (2)
Amefundisha Qur'ani
خَلَقَ الْإِنسَانَ (3)
Amemuumba mwanaadamu
عَلَّمَهُ الْبَيَانَ (4)
Akamfundisha kubaini
الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ بِحُسْبَانٍ (5)
Jua na mwezi huenda kwa hisabu
وَالنَّجْمُ وَالشَّجَرُ يَسْجُدَانِ (6)
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea
وَالسَّمَاءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ الْمِيزَانَ (7)
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani
أَلَّا تَطْغَوْا فِي الْمِيزَانِ (8)
Ili msidhulumu katika mizani
وَأَقِيمُوا الْوَزْنَ بِالْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا الْمِيزَانَ (9)
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani
وَالْأَرْضَ وَضَعَهَا لِلْأَنَامِ (10)
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe
فِيهَا فَاكِهَةٌ وَالنَّخْلُ ذَاتُ الْأَكْمَامِ (11)
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba
وَالْحَبُّ ذُو الْعَصْفِ وَالرَّيْحَانُ (12)
Na nafaka zenye makapi, na rehani
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (13)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
خَلَقَ الْإِنسَانَ مِن صَلْصَالٍ كَالْفَخَّارِ (14)
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo
وَخَلَقَ الْجَانَّ مِن مَّارِجٍ مِّن نَّارٍ (15)
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (16)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
رَبُّ الْمَشْرِقَيْنِ وَرَبُّ الْمَغْرِبَيْنِ (17)
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (18)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
مَرَجَ الْبَحْرَيْنِ يَلْتَقِيَانِ (19)
Anaziendesha bahari mbili zikutane
بَيْنَهُمَا بَرْزَخٌ لَّا يَبْغِيَانِ (20)
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (21)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
يَخْرُجُ مِنْهُمَا اللُّؤْلُؤُ وَالْمَرْجَانُ (22)
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (23)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
وَلَهُ الْجَوَارِ الْمُنشَآتُ فِي الْبَحْرِ كَالْأَعْلَامِ (24)
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (25)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ (26)
Kila kilioko juu yake kitatoweka
وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ (27)
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (28)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
يَسْأَلُهُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِي شَأْنٍ (29)
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (30)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
سَنَفْرُغُ لَكُمْ أَيُّهَ الثَّقَلَانِ (31)
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (32)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
يَا مَعْشَرَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ إِنِ اسْتَطَعْتُمْ أَن تَنفُذُوا مِنْ أَقْطَارِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ فَانفُذُوا ۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلْطَانٍ (33)
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (34)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
يُرْسَلُ عَلَيْكُمَا شُوَاظٌ مِّن نَّارٍ وَنُحَاسٌ فَلَا تَنتَصِرَانِ (35)
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (36)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
فَإِذَا انشَقَّتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ وَرْدَةً كَالدِّهَانِ (37)
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (38)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُسْأَلُ عَن ذَنبِهِ إِنسٌ وَلَا جَانٌّ (39)
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (40)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
يُعْرَفُ الْمُجْرِمُونَ بِسِيمَاهُمْ فَيُؤْخَذُ بِالنَّوَاصِي وَالْأَقْدَامِ (41)
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (42)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
هَٰذِهِ جَهَنَّمُ الَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا الْمُجْرِمُونَ (43)
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha
يَطُوفُونَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ حَمِيمٍ آنٍ (44)
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (45)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ جَنَّتَانِ (46)
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (47)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
ذَوَاتَا أَفْنَانٍ (48)
Bustani zenye matawi yaliyo tanda
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (49)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
فِيهِمَا عَيْنَانِ تَجْرِيَانِ (50)
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (51)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
فِيهِمَا مِن كُلِّ فَاكِهَةٍ زَوْجَانِ (52)
Humo katika kila matunda zimo namna mbili
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (53)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ فُرُشٍ بَطَائِنُهَا مِنْ إِسْتَبْرَقٍ ۚ وَجَنَى الْجَنَّتَيْنِ دَانٍ (54)
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (55)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
فِيهِنَّ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ (56)
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (57)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
كَأَنَّهُنَّ الْيَاقُوتُ وَالْمَرْجَانُ (58)
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (59)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
هَلْ جَزَاءُ الْإِحْسَانِ إِلَّا الْإِحْسَانُ (60)
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (61)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ (62)
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (63)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
مُدْهَامَّتَانِ (64)
Za kijani kibivu
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (65)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
فِيهِمَا عَيْنَانِ نَضَّاخَتَانِ (66)
Na chemchem mbili zinazo furika
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (67)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
فِيهِمَا فَاكِهَةٌ وَنَخْلٌ وَرُمَّانٌ (68)
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (69)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
فِيهِنَّ خَيْرَاتٌ حِسَانٌ (70)
Humo wamo wanawake wema wazuri
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (71)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
حُورٌ مَّقْصُورَاتٌ فِي الْخِيَامِ (72)
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (73)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
لَمْ يَطْمِثْهُنَّ إِنسٌ قَبْلَهُمْ وَلَا جَانٌّ (74)
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (75)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ رَفْرَفٍ خُضْرٍ وَعَبْقَرِيٍّ حِسَانٍ (76)
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ (77)
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
تَبَارَكَ اسْمُ رَبِّكَ ذِي الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ (78)
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu
❮ Previous Next ❯

Surahs from Quran :

1- Fatiha2- Baqarah
3- Al Imran4- Nisa
5- Maidah6- Anam
7- Araf8- Anfal
9- Tawbah10- Yunus
11- Hud12- Yusuf
13- Raad14- Ibrahim
15- Hijr16- Nahl
17- Al Isra18- Kahf
19- Maryam20- TaHa
21- Anbiya22- Hajj
23- Muminun24- An Nur
25- Furqan26- Shuara
27- Naml28- Qasas
29- Ankabut30- Rum
31- Luqman32- Sajdah
33- Ahzab34- Saba
35- Fatir36- Yasin
37- Assaaffat38- Sad
39- Zumar40- Ghafir
41- Fussilat42- shura
43- Zukhruf44- Ad Dukhaan
45- Jathiyah46- Ahqaf
47- Muhammad48- Al Fath
49- Hujurat50- Qaf
51- zariyat52- Tur
53- Najm54- Al Qamar
55- Rahman56- Waqiah
57- Hadid58- Mujadilah
59- Al Hashr60- Mumtahina
61- Saff62- Jumuah
63- Munafiqun64- Taghabun
65- Talaq66- Tahrim
67- Mulk68- Qalam
69- Al-Haqqah70- Maarij
71- Nuh72- Jinn
73- Muzammil74- Muddathir
75- Qiyamah76- Insan
77- Mursalat78- An Naba
79- Naziat80- Abasa
81- Takwir82- Infitar
83- Mutaffifin84- Inshiqaq
85- Buruj86- Tariq
87- Al Ala88- Ghashiya
89- Fajr90- Al Balad
91- Shams92- Lail
93- Duha94- Sharh
95- Tin96- Al Alaq
97- Qadr98- Bayyinah
99- Zalzalah100- Adiyat
101- Qariah102- Takathur
103- Al Asr104- Humazah
105- Al Fil106- Quraysh
107- Maun108- Kawthar
109- Kafirun110- Nasr
111- Masad112- Ikhlas
113- Falaq114- An Nas