القرآن باللغة السواحيلية - سورة العاديات مترجمة إلى اللغة السواحيلية، Surah Adiyat in Swahili. نوفر ترجمة دقيقة سورة العاديات باللغة السواحيلية - Swahili, الآيات 11 - رقم السورة 100 - الصفحة 599.

| وَالْعَادِيَاتِ ضَبْحًا (1) Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua | 
| فَالْمُورِيَاتِ قَدْحًا (2) Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini | 
| فَالْمُغِيرَاتِ صُبْحًا (3) Wakishambulia wakati wa asubuhi | 
| فَأَثَرْنَ بِهِ نَقْعًا (4) Huku wakitimua vumbi | 
| فَوَسَطْنَ بِهِ جَمْعًا (5) Na wakijitoma kati ya kundi | 
| إِنَّ الْإِنسَانَ لِرَبِّهِ لَكَنُودٌ (6) Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi | 
| وَإِنَّهُ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌ (7) Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo | 
| وَإِنَّهُ لِحُبِّ الْخَيْرِ لَشَدِيدٌ (8) Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali | 
| ۞ أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِي الْقُبُورِ (9) Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini | 
| وَحُصِّلَ مَا فِي الصُّدُورِ (10) Na yakakusanywa yaliomo vifuani | 
| إِنَّ رَبَّهُم بِهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّخَبِيرٌ (11) Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote |