| وَالشَّمْسِ وَضُحَاهَا (1) Naapa kwa jua na mwangaza wake
 | 
| وَالْقَمَرِ إِذَا تَلَاهَا (2) Na kwa mwezi unapo lifuatia
 | 
| وَالنَّهَارِ إِذَا جَلَّاهَا (3) Na kwa mchana unapo lidhihirisha
 | 
| وَاللَّيْلِ إِذَا يَغْشَاهَا (4) Na kwa usiku unapo lifunika
 | 
| وَالسَّمَاءِ وَمَا بَنَاهَا (5) Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga
 | 
| وَالْأَرْضِ وَمَا طَحَاهَا (6) Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza
 | 
| وَنَفْسٍ وَمَا سَوَّاهَا (7) Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza
 | 
| فَأَلْهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقْوَاهَا (8) Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake
 | 
| قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّاهَا (9) Hakika amefanikiwa aliye itakasa
 | 
| وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّاهَا (10) Na hakika amekhasiri aliye iviza
 | 
| كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِطَغْوَاهَا (11) Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao
 | 
| إِذِ انبَعَثَ أَشْقَاهَا (12) Alipo simama mwovu wao mkubwa
 | 
| فَقَالَ لَهُمْ رَسُولُ اللَّهِ نَاقَةَ اللَّهِ وَسُقْيَاهَا (13) Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake
 | 
| فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمْدَمَ عَلَيْهِمْ رَبُّهُم بِذَنبِهِمْ فَسَوَّاهَا (14) Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa
 | 
| وَلَا يَخَافُ عُقْبَاهَا (15) Wala Yeye haogopi matokeo yake
 |