القرآن باللغة السواحيلية - سورة المرسلات مترجمة إلى اللغة السواحيلية، Surah Mursalat in Swahili. نوفر ترجمة دقيقة سورة المرسلات باللغة السواحيلية - Swahili, الآيات 50 - رقم السورة 77 - الصفحة 580.

| وَالْمُرْسَلَاتِ عُرْفًا (1) Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole | 
| فَالْعَاصِفَاتِ عَصْفًا (2) Na zinazo vuma kwa kasi | 
| وَالنَّاشِرَاتِ نَشْرًا (3) Na zikaeneza maeneo yote | 
| فَالْفَارِقَاتِ فَرْقًا (4) Na zinazo farikisha zikatawanya | 
| فَالْمُلْقِيَاتِ ذِكْرًا (5) Na zinazo peleka mawaidha | 
| عُذْرًا أَوْ نُذْرًا (6) Kwa kuudhuru au kuonya | 
| إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَاقِعٌ (7) Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa | 
| فَإِذَا النُّجُومُ طُمِسَتْ (8) Wakati nyota zitakapo futwa | 
| وَإِذَا السَّمَاءُ فُرِجَتْ (9) Na mbingu zitakapo pasuliwa | 
| وَإِذَا الْجِبَالُ نُسِفَتْ (10) Na milima itakapo peperushwa | 
| وَإِذَا الرُّسُلُ أُقِّتَتْ (11) Na Mitume watakapo wekewa wakati wao | 
| لِأَيِّ يَوْمٍ أُجِّلَتْ (12) Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo | 
| لِيَوْمِ الْفَصْلِ (13) Kwa siku ya kupambanua | 
| وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الْفَصْلِ (14) Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (15) Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha | 
| أَلَمْ نُهْلِكِ الْأَوَّلِينَ (16) Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia | 
| ثُمَّ نُتْبِعُهُمُ الْآخِرِينَ (17) Kisha tukawafuatilizia walio fuatia | 
| كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ (18) Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (19) Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha | 
| أَلَمْ نَخْلُقكُّم مِّن مَّاءٍ مَّهِينٍ (20) Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa | 
| فَجَعَلْنَاهُ فِي قَرَارٍ مَّكِينٍ (21) Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti | 
| إِلَىٰ قَدَرٍ مَّعْلُومٍ (22) Mpaka muda maalumu | 
| فَقَدَرْنَا فَنِعْمَ الْقَادِرُونَ (23) Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (24) Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha | 
| أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ كِفَاتًا (25) Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya | 
| أَحْيَاءً وَأَمْوَاتًا (26) Walio hai na maiti | 
| وَجَعَلْنَا فِيهَا رَوَاسِيَ شَامِخَاتٍ وَأَسْقَيْنَاكُم مَّاءً فُرَاتًا (27) Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (28) Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha | 
| انطَلِقُوا إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ (29) Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha | 
| انطَلِقُوا إِلَىٰ ظِلٍّ ذِي ثَلَاثِ شُعَبٍ (30) Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu | 
| لَّا ظَلِيلٍ وَلَا يُغْنِي مِنَ اللَّهَبِ (31) Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako | 
| إِنَّهَا تَرْمِي بِشَرَرٍ كَالْقَصْرِ (32) Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba | 
| كَأَنَّهُ جِمَالَتٌ صُفْرٌ (33) Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (34) Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha | 
| هَٰذَا يَوْمُ لَا يَنطِقُونَ (35) Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu | 
| وَلَا يُؤْذَنُ لَهُمْ فَيَعْتَذِرُونَ (36) Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (37) Ole wao siku hiyo hao walio kanusha | 
| هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ ۖ جَمَعْنَاكُمْ وَالْأَوَّلِينَ (38) Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia | 
| فَإِن كَانَ لَكُمْ كَيْدٌ فَكِيدُونِ (39) Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (40) Ole wao siku hiyo hao walio kanusha | 
| إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي ظِلَالٍ وَعُيُونٍ (41) Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem | 
| وَفَوَاكِهَ مِمَّا يَشْتَهُونَ (42) Na matunda wanayo yapenda | 
| كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ (43) Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda | 
| إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ (44) Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (45) Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha | 
| كُلُوا وَتَمَتَّعُوا قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجْرِمُونَ (46) Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (47) Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha | 
| وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ارْكَعُوا لَا يَرْكَعُونَ (48) Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami | 
| وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ (49) Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha | 
| فَبِأَيِّ حَدِيثٍ بَعْدَهُ يُؤْمِنُونَ (50) Basi maneno gani baada ya haya watayaamini |