| حم (1) H'a Mim
 | 
| وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ (2) Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha
 | 
| إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ (3) Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji
 | 
| فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ (4) Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima
 | 
| أَمْرًا مِّنْ عِندِنَا ۚ إِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ (5) Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma
 | 
| رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ ۚ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ (6) Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua
 | 
| رَبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ (7) Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini
 | 
| لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْيِي وَيُمِيتُ ۖ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ (8) Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo
 | 
| بَلْ هُمْ فِي شَكٍّ يَلْعَبُونَ (9) Lakini wao wanacheza katika shaka
 | 
| فَارْتَقِبْ يَوْمَ تَأْتِي السَّمَاءُ بِدُخَانٍ مُّبِينٍ (10) Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri
 | 
| يَغْشَى النَّاسَ ۖ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٌ (11) Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu
 | 
| رَّبَّنَا اكْشِفْ عَنَّا الْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ (12) Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini
 | 
| أَنَّىٰ لَهُمُ الذِّكْرَىٰ وَقَدْ جَاءَهُمْ رَسُولٌ مُّبِينٌ (13) Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha
 | 
| ثُمَّ تَوَلَّوْا عَنْهُ وَقَالُوا مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ (14) Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu
 | 
| إِنَّا كَاشِفُو الْعَذَابِ قَلِيلًا ۚ إِنَّكُمْ عَائِدُونَ (15) Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile
 | 
| يَوْمَ نَبْطِشُ الْبَطْشَةَ الْكُبْرَىٰ إِنَّا مُنتَقِمُونَ (16) Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa
 | 
| ۞ وَلَقَدْ فَتَنَّا قَبْلَهُمْ قَوْمَ فِرْعَوْنَ وَجَاءَهُمْ رَسُولٌ كَرِيمٌ (17) Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu
 | 
| أَنْ أَدُّوا إِلَيَّ عِبَادَ اللَّهِ ۖ إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ (18) Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu
 | 
| وَأَن لَّا تَعْلُوا عَلَى اللَّهِ ۖ إِنِّي آتِيكُم بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ (19) Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi
 | 
| وَإِنِّي عُذْتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمْ أَن تَرْجُمُونِ (20) Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe
 | 
| وَإِن لَّمْ تُؤْمِنُوا لِي فَاعْتَزِلُونِ (21) Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami
 | 
| فَدَعَا رَبَّهُ أَنَّ هَٰؤُلَاءِ قَوْمٌ مُّجْرِمُونَ (22) Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu
 | 
| فَأَسْرِ بِعِبَادِي لَيْلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ (23) Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa
 | 
| وَاتْرُكِ الْبَحْرَ رَهْوًا ۖ إِنَّهُمْ جُندٌ مُّغْرَقُونَ (24) Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa
 | 
| كَمْ تَرَكُوا مِن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ (25) Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha
 | 
| وَزُرُوعٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ (26) Na mimea na vyeo vitukufu
 | 
| وَنَعْمَةٍ كَانُوا فِيهَا فَاكِهِينَ (27) Na neema walizo kuwa wakijistareheshea
 | 
| كَذَٰلِكَ ۖ وَأَوْرَثْنَاهَا قَوْمًا آخَرِينَ (28) Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe
 | 
| فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ السَّمَاءُ وَالْأَرْضُ وَمَا كَانُوا مُنظَرِينَ (29) La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula
 | 
| وَلَقَدْ نَجَّيْنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ مِنَ الْعَذَابِ الْمُهِينِ (30) Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha
 | 
| مِن فِرْعَوْنَ ۚ إِنَّهُ كَانَ عَالِيًا مِّنَ الْمُسْرِفِينَ (31) Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka
 | 
| وَلَقَدِ اخْتَرْنَاهُمْ عَلَىٰ عِلْمٍ عَلَى الْعَالَمِينَ (32) Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe
 | 
| وَآتَيْنَاهُم مِّنَ الْآيَاتِ مَا فِيهِ بَلَاءٌ مُّبِينٌ (33) Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi
 | 
| إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَيَقُولُونَ (34) Hakika hawa wanasema
 | 
| إِنْ هِيَ إِلَّا مَوْتَتُنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُنشَرِينَ (35) Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi
 | 
| فَأْتُوا بِآبَائِنَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ (36) Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli
 | 
| أَهُمْ خَيْرٌ أَمْ قَوْمُ تُبَّعٍ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ أَهْلَكْنَاهُمْ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا مُجْرِمِينَ (37) Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu
 | 
| وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَاعِبِينَ (38) Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo
 | 
| مَا خَلَقْنَاهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ (39) Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui
 | 
| إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ مِيقَاتُهُمْ أَجْمَعِينَ (40) Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote
 | 
| يَوْمَ لَا يُغْنِي مَوْلًى عَن مَّوْلًى شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ (41) Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa
 | 
| إِلَّا مَن رَّحِمَ اللَّهُ ۚ إِنَّهُ هُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ (42) Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu
 | 
| إِنَّ شَجَرَتَ الزَّقُّومِ (43) Hakika Mti wa Zaqqum
 | 
| طَعَامُ الْأَثِيمِ (44) Ni chakula cha mwenye dhambi
 | 
| كَالْمُهْلِ يَغْلِي فِي الْبُطُونِ (45) Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
 | 
| كَغَلْيِ الْحَمِيمِ (46) Kama kutokota kwa maji ya moto
 | 
| خُذُوهُ فَاعْتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَاءِ الْجَحِيمِ (47) (Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu
 | 
| ثُمَّ صُبُّوا فَوْقَ رَأْسِهِ مِنْ عَذَابِ الْحَمِيمِ (48) Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka
 | 
| ذُقْ إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْكَرِيمُ (49) Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu
 | 
| إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِ تَمْتَرُونَ (50) Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka
 | 
| إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٍ (51) Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani
 | 
| فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ (52) Katika mabustani na chemchem
 | 
| يَلْبَسُونَ مِن سُندُسٍ وَإِسْتَبْرَقٍ مُّتَقَابِلِينَ (53) Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana
 | 
| كَذَٰلِكَ وَزَوَّجْنَاهُم بِحُورٍ عِينٍ (54) Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini
 | 
| يَدْعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَاكِهَةٍ آمِنِينَ (55) Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani
 | 
| لَا يَذُوقُونَ فِيهَا الْمَوْتَ إِلَّا الْمَوْتَةَ الْأُولَىٰ ۖ وَوَقَاهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ (56) Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu
 | 
| فَضْلًا مِّن رَّبِّكَ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ (57) Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa
 | 
| فَإِنَّمَا يَسَّرْنَاهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ (58) Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka
 | 
| فَارْتَقِبْ إِنَّهُم مُّرْتَقِبُونَ (59) Ngoja tu, na wao wangoje pia
 |